Home Uncategorized BUSUNGU AWAOMBA WATANZANIA KUENDELEA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA

BUSUNGU AWAOMBA WATANZANIA KUENDELEA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA

MAALIM Busungu mshambuliaji wa z

amani wa Yanga amesema kuwa kwa sasa ni muhimu kila mmoja akachukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona.

Busungu amesema kuwa hali inaweza kuwa salama iwapo kila mmoja akachukua tahadhari dhidi Corona na kujilinda yeye kwanza na jamii kiujumla.

 “Kwa kipindi hiki kigumu ambacho tunapitia ni muhimu kila mmoja akachukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona kwani ni janga hatari ambalo linaitikisa dunia.

 “Iwapo kila mmoja akachukua tahadhari itakuwa rahisi kwake kujilinda na kuwalinda wengine, yale malelekezo yanayotolewa na Wizara ya afya pamoja na Serikali yasipuuzwe,” amesema.

SOMA NA HII  A-Z KUHUSU ISHU YA KAKOLANYA SIMBA IPO NAMNA HIVI