Home Uncategorized HAWA NSIO SINGIDA UNITED NA MWENDO WAO

HAWA NSIO SINGIDA UNITED NA MWENDO WAO


SINGIDA United ya mkoani Singida ikiwa chini ya Kocha Mkuu Ramadhan Nswanzurimo ipo nafasi ya 20 ndani ya Ligi Kuu Bara msimu wa 2019/20.

Ikiwa imecheza jumla ya mechi 29 ambazo ni dakika 2,610 kibindoni imejikusanyia pointi 15.

Imeshinda mechi tatu ambazo ilikuwa ni mbele ya Ruvu Shooting na Mbeya City haikuwa na bahati kwani imepigwa nje ndani.

Imefunga mabao 16 huku ikikubali kubebeshwa zigo la mabao 49 kichapo kikubwa ilichobeba kwa msimu huu ni mbele ya Simba Uwanja wa Uhuru ilipokubali kuchapwa mabao 8-0.

SOMA NA HII  MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA SPOTI XTRA ALHAMISI