Home Uncategorized MAMBO BADO HAYAJAWA SHWARI NDANI YA ENGLAND

MAMBO BADO HAYAJAWA SHWARI NDANI YA ENGLAND



TIMU zinazoshiriki Ligi Kuu England kesho zinatarajiwa kupiga kura kuhusu maamuzi ya kurejea rasmi kwenye mazoezi ya pamoja ili kujiaandaa kumaliza msimu wa 2019/20.
Kwa sasa kumekuwa na hofu ya kuanza mazoezi ya pamoja kutokana na janga la Virusi la Corona ambalo linaivurugavuruga dunia na kufanya shughuli nyingi zisimamishwe kuepuka maambukizi zaidi.
Mpango uliopo ni kuona kwamba ligi inarejea Juni ili kumaliza mechi ambazo zimebaki huku timu zote 20 zikitarajiwa kupiga kura kesho.
Kwa sasa timu zimeruhusiwa kufanya mazoezi lakini wanafanya kwa makundimakundi ili kuendelea kuchukua tahadhari ya Virusi vya Corona na kuna baadhi ya wachezaji ambao wameamua kutojihusisha kabisa na mazoezi kutokana na hofu waliyonayo.
Timu nyingi zinaamini kwamba itakuwa ngumu kucheza hivi karibuni kutokana na wachezaji wao wa kikosi cha kwanza kuwa na hofu ya Corona na wengine wakiwa wanaumwa jambo ambalo linafanya hofu izidi kutanda.
Baadhi ya nyota ambao wamejiengua kwenye mazoezi ya timu ni pamoja na kiungo wa Chelsea, N’Golo Kante na Troy Deeney nahodha wa Watford.

SOMA NA HII  KOCHA WA SIMBA AWAKOMALIA WACHEZAJI WAKE KUPIGA MATIZI