BAADA ya jana Azam FC kutoshana nguvu na Trasint Camp kwenye mchezo wa kirafiki sasa nguvu zote zinaelekezwa kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mbao.
Jana, Azam FC ilianza kutesti mitambo baada ya kukaa bila kucheza mechi ya ushindani tangu Machi 17 kutokana na Serikali kusimamisha masuala ya michezo ili kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona.
Tayari masuala ya michezo yameruhusiwa na Serikali baada ya kueleza kuwa hali ya maambukizi imepungua.
Juni 14 Azam FC iliyo chini ya Aristica Cioaba itaendelea ratiba zake za Ligi Kuu Bara kwa kumenyana na Mbao FC, Uwanja wa Azam Complex.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.