Home Uncategorized KIUNGO FUNDI ANAYEZIGOMBANISHA SIMBA NA YANGA ATAJA ATAKAPOSAINI

KIUNGO FUNDI ANAYEZIGOMBANISHA SIMBA NA YANGA ATAJA ATAKAPOSAINI

BARAKA Majogoro ni kiungo mkabaji ndani ya Klabu ya Polisi Tanzania iliyo chini ya Kocha Mkuu Malale Hamsini.

Jina lake linatajwa mitaa ya Kariakoo ambapo inaelezwa kuwa Simba na Yanga wanahitaji kupata saini yake.

Kwenye sarakasi za dirisha dogo Simba ilikwama kupata saini ya kiungo huyu na inaelezwa kuwa nafasi yake ikachukuliwa na Shiza Kichuya.

Thamani yake inatajwa kuwa milioni 30 ili kumpata na kwa sasa anamalizia kandarasi yake ndani ya Polisi Tanzania. 

Majogoro amesema:”Kwangu mimi iwe Yanga ama Simba fresh. Kikubwa nafasi yangu ndani ya timu pamoja na makubaliano mazuri.

 “Kila kitu ni maelewano, kazi yangu ni kucheza na utaratibu upo wazi ni lazima ufuatwe.”

SOMA NA HII  SIMBA KUSHUKA UWANJANI KESHO KUMENYANA NA AFRICAN LYON