Home Uncategorized LIGI KUU YA ZANZIBAR KUPIGWA KWENYE KITUO KIMOJA NA HAKUNA MASHABIKI

LIGI KUU YA ZANZIBAR KUPIGWA KWENYE KITUO KIMOJA NA HAKUNA MASHABIKI


KATIBU Mkuu Wizara ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hassan Omar Hassan King, amesema Ligi kuu Zanzibar, itachezwa katika kituo kimoja cha Unguja ili kupunguza timu kusafiri pamoja na gharama nyingine za uendeshaji timu.

Akizungumza na Waandishi wa Habari, ameeleza kwamba, Serikali imefikia uamuzi huo kwa lengo la kujikinga na virusi vya Corona.


Ameongeza kuwa katika ligi hiyo hakutakuwa na mashabiki watakaoruhusiwa kuingia uwanjani ili kuchukua tahadhari zaidi ya janga la Corona.

Viwanja viwili vitatumika kwenye mechi zote zilizobaki ikiwa ni Uwanja wa Aman na Mau. Ligi ya Zanzibar ilisimamishwa tangu Machi 17.

SOMA NA HII  ISHU YA JONAS MKUDE WA SIMBA KUSAINI YANGA IPO HIVI