MASAU Bwire, Ofisa Habari wa Ruvu Shooting amesema kuwa waliokuwa wanawabeza baada ya kupokea kichapo cha mabao 2-1 mbele ya KMC wasitarajie watafungwa leo mbele ya Ndanda FC.
Ndanda inayonolewa na Kocha Mkuu, Meja Mstaafu, Abdul Mingange itashuka uwanjani ikiwa na kumbukumbu ya kushinda bao 1-0 mbele ya Biashara United, Uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Leo, Juni 23, Ruvu Shooting itakuwa na kazi ya kumenyana na Ndanda Uwanja wa Mabatini, majira ya saa 10:00 jioni huku tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona ikiendelea kuchukuliwa.
“Niwakumbushe kwamba ukiachana na sare tuliyopata mbele ya Simba, tulifungwa mabao 2-1 na KMC ila haina maana kwamba na leo tutafungwa na Ndanda hilo halipo, muhimu kujua kwamba tunaendelea kupapasa.
“Kocha Mkuu, Salum Mayanga amenihakikishia kwamba wapo vizuri na wachezaji wana morali kubwa hivyo hakuna cha kuhofia mashabiki wajitokeze kuona namna gani Barcelona ya Bongo inatoa burudani,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.