Home Uncategorized MWENDO WA SAMATTA AKILINI MWA BUSUNGU

MWENDO WA SAMATTA AKILINI MWA BUSUNGU

Na: Saleh Ally
UKITULIA utaona kuwa suala la vipaji wakati mwingine sisi wenyewe Watanzania huwa tunaviua vya kwetu.

Huyu mwana yaani Busungu kamaliza kipaji chake, tokea alipoifunga Simba akiwa Yanga basi alianza kuporomoka tu maana aliona amemaliza ndoto yake.

Nilikuwa navutiwa na aina yake ya uchezaji na niliamini angefika mbali ndio maana nilishiriki kuona siku moja anarejea lakini kiuhalisia, imeshindikana tayari.

Kuifunga Simba kulimfanya aone hana kazi nyingine mbele yake. Sasa ataendelea kushuka madaraja na ukubwa au haishi na timu hadi hapo atakapoanza kulaumu ALIONEWA.

Hakuna aliyemuonea, kajionea mwenyewe na inaonekana wazi kuwa nafasi ya yeye kurudi katika kiwango cha Busungu hatari imeshindikana.

Busungu aliibuka baada ya Mbwana Samatta, nakumbuka wakati anaanza kutamba Samatta alikuwa TP Mazembe na leo yuko Aston Villa Busungu.


SOMA NA HII  SIMBA YAJIFUA LEO SUMBAWANGA KUELEKEA MCHEZO WA FAINALI KOMBE LA SHIRIKISHO