Home Uncategorized UWANJA WA SIMBA WAPIGWA PINI NA TFF

UWANJA WA SIMBA WAPIGWA PINI NA TFF


SHIRIKISHO la Soka Tanzania, (TFF) limeupiga pini Uwanja wa Simba Mo Arena kwa matumizi ya mechi za kirafiki.

Jana, Juni 7 Uwanja huo ulitumika kwa mechi ya kirafiki kati ya Simba na KMC ambapo Simba ilishinda mabao 3-1.

TFF imesema kuwa uwanja huo utatumika kwa ajili ya mazoezi na sio mechi za ushindani.

Sababu kubwa ni kuendelea kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona na kuzitaka timu zitakapoandaa mechi kuzingatia muongozo uliotolewa na Serikali.

SOMA NA HII  MZUNGU WA YANGA AMPA PROGRAMU MAALUMU ALIYEWABINA KAGERE NA BOCCO