Home Uncategorized MO DEWJI AMWAGA MAMILIONI SIMBA IKIIUA YANGA KESHO..!!!

MO DEWJI AMWAGA MAMILIONI SIMBA IKIIUA YANGA KESHO..!!!

SIMBA bado wanalikumbuka lile bao la friikiki ya Bernard Morrison kwenye mchezo wao wa mwisho wa Ligi Kuu Bara na jinsi lilivyowatese mbele ya mashabiki wa Yanga, lakini sasa unaambiwa zikiwa zimesalia siku chache kabla ya timu hizo kukutana tena, bilionea wao, Mohammed ‘Mo’ Dewji ameamua kufanya yake, ili kuhakikisha Jumapili wanapindua meza kibabe mbele ya watani wao.

Simba na Yanga zitavaana kwenye mechi ya nusu fainali ya Kombe la Shirikisho (ASFC) itakayopigwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam kuamua timu ya kucheza fainali na bilionea huyo kijana aliyepia pia Mwenyekiti wa Bodi ya Simba, amewajaza upepo nyota wake kwa kuwamwagia mamilioni.

Katika mchezo wao wa mwisho ambao Simba ililala 1-0, nyota wa Yanga walipewa mzuka kwa kumwagiwa kiasi cha Sh200 milioni kama sehemu ya motisha na kweli mnyama akafa Taifa, lakini safari hii mabosi wa Msimbazi wameamua kujibu mapigo ili kumaliza tambo za Morrison.

Habari za kuaminika kutoka ndani ya Simba zinasema, Mo Dewji amepanga kuwapa donge nono nyota wake kama wataifunga Yanga na kuwatibulia kupata tiketi ya ushiriki wa michuano ya kimataifa mwakani, ikiwa ndio nafasi pekee kwa Jangwani kushiriki michuano ya CAF.

Tiketi ya Ligi ya Mabingwa Afrika tayari ipo mkononi mwa Simba iliyotwaa ubingwa wa Ligi Kuu kwa msimu wa tatu mfululizo, huku Yanga ikipambana na Azam FC na Namungo kuwania kumaliza nafasi ya pili kama ilivyokuwa msimu uliopita.

Mmoja wa vigogo wa Simba ameliopenyezea Mwanaspoti, bilionea huyo ametoa ahadi ya kuwapa nyota wa timu hiyo Dola za Kimarekani 100,000 ambazo ni zaidi ya Sh230 milioni kwa Fedha za Kitanzania.

SOMA NA HII  KIKOSI CHA YANGA KITAKACHOANZA LEO DHIDI YA TANZANIA PRISONS