UONGOZI wa Simba umesema kuwa hauna mpango na mchezaji matata wa Yanga, Bernard Morrison ambaye amekuwa akitajwa kuhitajiwa na Simba.
Ilikuwa inaelezwa kuwa Simba walikuwa wanahitaji huduma ya Morrison ambaye aliwatungua walipokutana Uwanja wa Taifa, Machi 8 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara ambapo Simba ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0.
Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa Simba wana wachezaji wengi wazuri na hawana mpango wa kumvuta ndani ya kikosi cha Simba.
“Hakuna, hakuna mpango wa Simba kuzungumza na Morrison, tunatambua kwamba tupo imara na hatuwezi kuzungumza na mchezaji huyo licha ya kwamba yupo vizuri.
“Ninawajua wachezaji wazuri ila hayupo kwenye mipango yetu kwa sasa hayo yanayozungumzwa ni maneno tu hamna kitu kingine,” amesema.
Chanzo:Wasafi
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.