Home Uncategorized KICHUYA ATAJA SABABU YA ‘KUBUMA’ SIMBA

KICHUYA ATAJA SABABU YA ‘KUBUMA’ SIMBA

Habari za Yanga


KIUNGO mshambuliaji wa Namungo FC, Shiza Kichuya anasema bado ana matumaini ya kurejea kwenye kiwango cha juu kama ilivyokuwa zamani huku akisema kuwa ukosefu wa namba ndani ya Simba ni miongoni mwa sababu zilizomfanya akasepa.

 

Kichuya amejiunga kwa mkataba wa miaka miwili kwenye kikosi hicho chenye maskani yake Ruangwa mkoani Lindi akitokea Simba, anasema kikubwa ni kujituma na kufanya mazoezi kwa bidii.

 

“Naamini kuna wachezaji wazuri zaidi ndani ya Namungo, hivyo natakiwa kupambana ili kumwaminisha kocha na kunipatia nafasi ya kila mara kucheza kwenye kikosi cha kwanza.

 

“Namungo ni timu kubwa ndio maana nimekuja huku, nikifanikiwa kupata namba kila wakati naamini kila mmoja atafurahi kwa kile nitakachokifanya uwanjani,” anasema Kichuya.

 

Mshambuliaji huyo ameongoza kusema licha ya mkataba wake kumalizika ndani ya Simba lakini ukosefu wa namba umechangia kuondoka kwake.


Akiwa Simba msimu wa 2019/20 alifunga bao moja kati ya mabao78 yaliyofungwa na timu hiyo ilikuwa Uwanja wa Mkapa wakati timu yake ikilazimisha sare ya kufungana bao 1-1 na Ruvu Shooting.

SOMA NA HII  MZAHA KWENYE CORONA NA PROGRAMU ZA WACHEZAJI USIPEWE NAFASI