Home Uncategorized MAJEMBE MAPYA YA YANGA KUTUA MAPEMA KABLA YA SEPTEMBA SITA

MAJEMBE MAPYA YA YANGA KUTUA MAPEMA KABLA YA SEPTEMBA SITA

 


BAADA ya Yanga kumalizana na majembe mawili ya kazi kwa dili la miaka miwili jana, Agosti 17 nchini Congo nyota hao wanatarajiwa kutua kesho, Dar kuungana na wachezaji wenzao ambao wameshaanza maandalizi ya msimu wa 2020/21.


Mkurugenzi wa Uwekezaji ndani ya Kampuni ya GSM, Injinia Hersi Said ndiye amekamilisha mpango wa nyota hao kuibukia ndani ya Yanga.

Mukoko Tonombe ambaye ni mshambuliaji na mwenzake Tuisila Kisinda wote walikuwa wanakipiga ndani ya Klabu ya AS Vita, ya Congo.

Agosti 20, ambayo itakuwa ni siku ya Alhamisi wachezaji hao wanatarajiwa kutua timu Bongo kuungana na nyota wengine ambao walianza mazezi Agosti 10.

Septemba sita, Ligi Kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuanza na Yanga itaanza kurusha kete yake ya kwanza mbele ya Tanzania Prisons Uwanja wa Mkapa.
SOMA NA HII  MUONEKANO WA UKURASA WA MBELE GAZETI LA CHAMPIONI IJUMAA