Home Uncategorized MKALI WA KUCHEKA NA NYAVU ANUKIA JANGWANI

MKALI WA KUCHEKA NA NYAVU ANUKIA JANGWANI

Wazir Jr nyota wa kikosi cha Mbao FC anatajwa kumalizana na Klabu ya Yanga ambayo inapambana kuboresha kikosi chake kwa sasa.

Junior ni kinara wa utupiaji ndani ya Mbao FC akiwa ametupia mabao 12 ndani ya Ligi Kuu Bara na mabao mawili kwenye mchezo wa playoffs dhidi ya Ihefu FC.

Mbao FC imefungwa jumla ya mabao 4-4 na Ihefu jambo lililowafanya Mbao msimu ujao kushiriki Ligi Daraja la Kwanza.

Mbao imetolewa kwa mabao  ya ugenini ambayo Ihefu iliwafunga jana Agosti Mosi, Uwanja wa Kirumba.

SOMA NA HII  HESABU ZA SIMBA NI KWA WANIGERIA, SVEN ATOA NENO