Home Uncategorized NYOTA HAWA WANNE WA KIKOSI CHA KWANZA SIMBA KUIKOSA NAMUNGO LEO

NYOTA HAWA WANNE WA KIKOSI CHA KWANZA SIMBA KUIKOSA NAMUNGO LEO


 LEO Agosti 30, Simba inashuka Uwanja wa Amri Sheikh Abeid kumenyana na Klabu ya Namungo kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii utakaopigwa majira ya 9:00 alasiri.


Mchezo huu ni maalumu kwa ajili ya ufunguzi wa Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza Septemba sita.


Simba inayonolewa na Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck inatarajiwa kukosa huduma ya nyota wake wa kikosi cha kwanza wanne kutokana na sababu mbalimbali kwa mujibu wa kocha mwenyewe ambao ni:-

Beki wa kati raia wa Ivory Coast, Pascal Wawa.


Luis Miqussone kiungo mshambuliaji raia wa Msumbiji.


Gerson Fraga kiungo mkabaji raia wa Brazili na Chris Mugalu yeye ni mshambuliaji.

SOMA NA HII  KOCHA YANGA ADAI KULIKUWA NA HARUFU ISIYOFAA VYUMBANI