Home Uncategorized KAGERA SUGAR V YANGA NI BALAA TUPU, REKODI ZAIGOMEA SARE

KAGERA SUGAR V YANGA NI BALAA TUPU, REKODI ZAIGOMEA SARE


LEO Kagera Sugar inawakaribisha Yanga kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuchezwa majira ya saa 10:00 jioni.


Ni mchezo wa kwanza kwa Yanga nje ya Dar huku kwa Kagera Sugar ukiwa ni wa pili kucheza Uwanja wa Kaitaba.


Rekodi zinaonyesha kuwa ndani ya misimu mitatu ya hivi karibuni, Kagera Sugar na Yanga zikiwa zimekutana mara sita, Kagera Sugar imeshinda mara moja huku wakiwa hawajaambulia sare na Yanga imeshinda mara tano.


Jumla Yanga imefunga mabao 11 huku Kagera Sugar ikifunga mabao sita kati ya mabao 17 ambayo yamefungwa kwa wababe hawa.


Hivyo mchezo wa leo unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kwa kuwa rekodi zinaonyesha kwamba kupatikana sare kwa timu hizi mbili kwa misimu ya hivi karibuni imekuwa ni ngumu.

 Misimu mitatu nyuma matokeo ya Kagera Sugar v Yanga matoke yapo namna hii:-


2019/20

Kagera Sugar 0-1 Yanga

Yanga 0-3 Kagera Sugar

2018/19

Yanga 3-0 Kagera Sugar
Kagera Sugar 1-2 Yanga

2017/17
Yanga 3-0 Kagera Sugar
Kagera Sugar 1-2 Yanga.

SOMA NA HII  MTAALAMU WA SOKA LA KISASA YANGA ASEPA ZAKE KWAO, KILICHOFANYIKA CHATAJWA