Mohamed Banka, kiungo wa zamani wa Klabu ya Yanga na Simba amepatwa na msiba kwa kuondokewa na mkewe, Bi Mariam Abdul Banchu.
Umauti umemfikia Mariam usiku wa kuamkia leo kwenye Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam baada ya kujiskia vibaya ghafla na kupelekwa kupewa huduma mpaka kukutwa na umauti.
Shughuli za mazishi zitafanyika kwenye msikiti wa Maamur na maziko yatafanyika makaburi ya Kisutu na msiba utakuwa Tabata Chang’ombe.