Home Uncategorized WAJUMBE WAMPOTEZA DROGBA NAFASI YA URAIS FIF

WAJUMBE WAMPOTEZA DROGBA NAFASI YA URAIS FIF


 KAMATI ya uchaguzi ya shirikisho la soka Ivory Coast (FIF) imemuengua mchezaji wa zamani wa Chelsea na timu ya taifa ya Ivory Coast Didier Drogba katika kinyang’anyiro cha kuwania Urais wa FIF kwa sababu ya kudaiwa document zake hazikukidhi vigezo.

 

Drogba inadaiwa ndio anapewa kipaumbele zaidi katika mbio za kuwania Urais wa FIF katika uchaguzi mkuu wa FIF unaotarajia kufanyika Septemba, 5 2020.

 

Kwa kuenguliwa huko basi Drogba anapoteza nafasi ya kuwania nafasi ya Urais na kumuacha Sory Diabate na Idriss Diallo katika mbio za kuwani urais huo.


Drogba alikuwa akipewa nafasi kubwa ya kuwa kiongozi katika uchaguzi huo ila wajumbe ndo wamempa alichostahili staa huyo wa zamani wa Klabu ya Chelsea.


SOMA NA HII  WATU WAENDELEA KUCHOTA MKWANJA NDANI YA SPORTPEA, CHALII AONDOKA NA MILIONI 6 NA USHEE