Home Uncategorized AZAM FC YAINYOOSHA KWA BAO 1-0 MBEYA CITY

AZAM FC YAINYOOSHA KWA BAO 1-0 MBEYA CITY

 


ALLY Niyonzima nyota mpya wa Azam FC aliyeibukia huko akitokea Klabu ya Rayon Sports ya Rwanda leo amepachika bao lake la kwanza wakati wakishinda kwa bao 1-0 mbele ya Mbeya City.

Mchezo huo umechezwa leo Septemba 20, Uwanja wa Sokoine ni wa tatu kwa Mbeya City kupoteza na wa tatu kwa Azam kushinda.


Niyonzima amefungua akaunti yake ya mabao leo dakika ya 24 kwa kupachika bao lake kwa kichwa akiwa ndani ya 18.

Jumla Azam FC imeshinda mechi tatu ikiwa na pointi 9 kibindoni nafasi ya kwanza na Mbeya City nafasi ya 18 na haijaambulia pointi kibindoni.
SOMA NA HII  AZAM FC KUMBE WAMEYEYUSHA POINTI 15 KISA WAAMUZI