Home Uncategorized JAMES RODRIGUEZ MALI YA EVERTON

JAMES RODRIGUEZ MALI YA EVERTON



RASMI sasa, James Rodriguez raia wa Columbia atakipiga ndani ya Klabu ya Everton baada ya kusaini dili la miaka miwili kwa dau la thamani ya paundi milioni 20.

James  amekubali kusaini dili hilo ndani ya Everton inayoshiriki Ligi Kuu England, dili hilo lina kipengele cha kuongeza mkataba wake ikiwa ataonyesha ubora ndani ya msimu wake wa kwanza.

Atakuwa chini ya Kocha Mkuu, Carlo Ancelotti ambaye anakiongoza kikosi hicho kinachotumia Uwanja wa Goodison Park.


Nyota huyo mwenye miaka 29 alikuwa anakipiga Klabu ya Bayern Munich inayoshiriki Bundesliga kwa mkopo msimu wa 2017/19 akitokea Klabu ya Real Madrid aliyoichezea jumla ya mechi 85 na kufunga mabao 29.

Ancelotti amesema kuwa anatambua vema uwezo wa kiungo huyo tangu akiwa ndani ya Real Madrid na Bayern Munich jambo linalomfanya aamini kwamba atakuwa bora ndani ya kikosi chake.

James amesema’ Nina furaha kuwa hapa ninapenda kuvaa jezi hii ya rangi ya bluu,”.


:

SOMA NA HII  SERIKALI YAZUIA MASHABIKI WA SIMBA KUSHEREKEA UBINGWA