Home Uncategorized MASHINE MPYA 10 ZA DODOMA FC HIZI HAPA

MASHINE MPYA 10 ZA DODOMA FC HIZI HAPA


LIGI Kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 6 kwa timu 18 kuanza mbio za kulisaka taji la ligi lililo mikononi mwa Simba.


Tayari dirisha la usajili liifungwa Agosti 31 baada ya kufunguliwa Agosti Mosi na lilikuwa ni kwa muda wa mwezi mmoja kutokana na janga la Virusi vya Corona kutibua mambo.


Dodoma FC inayonolewa na Mbwana Makata, imepanda kutoka Ligi Daraja la Kwanza ikitokea kundi A baada ya kufikisha jumla ya pointi 51 itafungua pazia lake kwa kumenyana na Mwadui FC, Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, Septemba 6:-


Haya hapa ni majembe mapya 10 ndani ya Dodoma FC

 Cleophace Mkandala kiungo kutoka Tanzania Prisons.

Michael Chinedu kutoka Alliance yeye ni mshambuliaji.

Seif Karihe kutoka Lipuli yeye ni kiungo mshambuliaji.

Peter Mapunda kutoka Mbeya City yeye ni mshambuliaji.

 Aron Kalambo kutoka Mbeya City yeye ni mlinda mlango.

Jukumu Kibanda, beki kutoka Namungo.

Justine Omari kutoka Klabu ya Biashara United yeye ni kiungo mkabaji.

Dickson Ambundo,akitokea Klabu ya Gor Mahia ya Kenya yeye ni winga.

Salmin Hoza yeye ni kiungo alijiunga na Dodoma FC akitokea Azam FC kwa mkopo.

 George Wawa aliibukia ndani ya Dodoma akitokea Klabu ya Singida United yeye ni beki


SOMA NA HII  SABABU ZA UWANJA WA AZAM COMPLEX KUWA SAWA NA TP MAZEMBE HIZI HAPA