LIGI Kuu Tanzania Bara inatarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 6 kwa timu 18 kuanza mbio za kulisaka taji la ligi lililo mikononi mwa Simba.
Tayari dirisha la usajili liifungwa Agosti 31 baada ya kufunguliwa Agosti Mosi na lilikuwa ni kwa muda wa mwezi mmoja kutokana na janga la Virusi vya Corona kutibua mambo.
Dodoma FC inayonolewa na Mbwana Makata, imepanda kutoka Ligi Daraja la Kwanza ikitokea kundi A baada ya kufikisha jumla ya pointi 51 itafungua pazia lake kwa kumenyana na Mwadui FC, Uwanja wa Jamhuri, Dodoma, Septemba 6:-
Haya hapa ni majembe mapya 10 ndani ya Dodoma FC
Cleophace Mkandala kiungo kutoka Tanzania Prisons.