Home Uncategorized BADO ANAKUMBUKWA HISTORIA YAKE ITABAKI PALEPALE SIR FERGUSON

BADO ANAKUMBUKWA HISTORIA YAKE ITABAKI PALEPALE SIR FERGUSON


KWENYE maisha yake ya kuwa Kocha Mkuu, jana, Mei 8, 2013 miaka saba iliyomeguka alitangaza kustaafu kwenye nafasi yake aliyokuwa.

 Sir Alex Ferguson alitangaza kujiuzulu kuwa Kocha Mkuu baada ya kudumu Kwenye nafasi hiyo kwa muda wa miaka 26 hivyo leo Mei 9 ilikuwa ni siku yake ya kwanza kuanza kuitumikia akiwa huru bila presha za masuala ya michezo.

Amesimamia mechi 1,500 ameshinda 895 sare 338 kipigo 267.

Mataji ya Ligi Kuu England kabatini 13, FA mataji matano, UCL mataji mawili, FIFA CWC taji moja, EFL mataji manne, Ngao ya Jamii mataji 10.


Bado anaendelea kukumbukwa na historia yake itabaki palepale mtu wa mipango hatari ndani ya uwanja huku mdomoni akiwa anatafuna big g, anaendelea kutoa sapoti ndani ya Manchester United ila hawezi kurejea tena kwenye benchi la ufundi kama zamani, muda unakwenda kasi sana.

SOMA NA HII  HILI HAPA JESHI ZIMA LA MAUAJI LA LIPULI FC MSIMU MPYA