Home Uncategorized MESSI ANAWEZA KUIKOSA EL CLASICO NDANI YA BARCELONA

MESSI ANAWEZA KUIKOSA EL CLASICO NDANI YA BARCELONA


 KOCHA mkuu wa Barcelona, Ronaldo Koeman huenda anaweza kuikosa huduma ya nyota wake Lionel Messi raia wa Argentina kwenye mechi tatu za La Liga ikiwa nyota atakwenda kwenye majukumu ya Taifa mwezi ujao.


Miongoni mwa mchezo ambao unampasua kichwa Kocha Mkuu wa Barcelona, Koeman ni pamoja na ule utakaowakutanisha dhidi ya Real Madrid maarufu kama El Clasico kwa mwezi Oktoba.


Ratiba inaonyesha kuwa mechi za timu ya Taifa ya Argentina kutafuta tiketi ya kufuzu Kombe la Dunia 2022 itakuwa ni Oktoba 8 ambapo itacheza na Ecoador na Oktoba 13 dhidi ya Bolivia.

Kwa mujibu wa kanuni nchini Hispania kwa sasa ni lazima kwa kila mmoja anayetoka Kusini mwa America lazima akae karantini kwa muda wa siku 14 hivyo kwa wakati huo Messi atakuwa hana namna ya kucheza mechi za La Liga.

Anaweza kukosa mechi dhidi ya Getafe na Alaves pia na kwa namna ratiba ilivyo anaweza kuikosa mechi kali dhidi ya Real Madrid maarufu kama El Clasico.

SOMA NA HII  VPL: KAGERA SUGAR 0-0 YANGA