Home Uncategorized NAMUNGO FC:BADO TUNA NAFASI YA KUFANYA VIZURI

NAMUNGO FC:BADO TUNA NAFASI YA KUFANYA VIZURI

 


BIGIRIMAMA Blaise mshambuliaji namba moja ndani ya Klabu ya Namungo FC amesema kuwa wanaamini watarejea kwenye ubora wao licha ya kupoteza mechi mbiili mfululizo. 


Namungo FC ilianza kwa ushindi mbele ya Coastal Union mchezo uliochezwa Uwanja wa Majaliwa na Blaise aliweka rekodi ya kuwa mfungaji wa kwanza ndani ya  Ligi kwa msimu wa 2020/21 kwa pasi ya Nurdin Barola ambaye ni kipa namba moja wa timu hiyo.


Mechi zao mbili mbele ya Polisi Tanzania ikiwa Uwanja wa Majaliwa na ule wa pili dhidi ya Prisons Uwanja wa Nelson Mandela ilipoteza kwa kuchapwa bao mojamoja.


Blaise amesema:Bado ligi inaanza kwa sasa tuna mechi nyingi mbele ambazo ni ngumu na za ushindani,  tutapambana kupata matokeo mazuri ili kujiweka nafasi nzuri.


“Mashabiki waendelee kutupa sapoti bila kukata tamaa imani ni kwamba kila kitu kitakuwa sawa ni matokeo ndani ya uwanja tunayopata kwa sasa,” amesema.

SOMA NA HII  HOFU YA TAMBWE IPO KWA MEDDIE KAGERE