Home Uncategorized BURUNDI WATIA TIMU BONGO, TAYARI KUIVAA STARS

BURUNDI WATIA TIMU BONGO, TAYARI KUIVAA STARS

 


TIMU ya Taifa ya Burundi tayari imewasili Bongo leo Oktoba 7 kamili kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa ulio kwenye kalenda ya FIFA.


Mchezo huo unatarajiwa kuchezwa Oktoba 11, Uwanja wa Mkapa na unatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na timu zote mbili kuwa na wachezaji wazuri.

 Pia ndani ya timu ya Burundi kuna wachezaji ambao wanacheza Ligi Kuu Bara jambo ambalo linaongeza ushindani kwa kuwa wanatambua soka la Bongo na falsafa zake.


Miongoni mwa nyota hao ni Bigirimana Blaise, Jonathan Nahimana wanakipiga ndani ya Namungo FC.

SOMA NA HII  AZAM FC YAZIPIGIA HESABU POINTI TATU ZA BIASHARA UNITED