Home Uncategorized MWAKINYO AMCHAPA KWA TKO MUARGENTINA

MWAKINYO AMCHAPA KWA TKO MUARGENTINA


HASSAN Mwakinyo, bondia Mtanzania amesema kuwa alijipanga kuibuka na ushindi mbele ya mpinzani wake Jose Carlos Pazi wa Argentina jambo lililompa ushindi.


 Bondia Mwakinyo usiku wa kuamika leo  amefanikiwa kuetetea mkanda wake wa WBF Intercontinental Super Welterweight.


Mwakinyo amemchapa Paz wa Argentina kwa TKO raundi ya nne kwenye Ukumbi wa Next Door Arena.


“Nilikuwa nimejipanga kushinda na ninafurahi kushinda katika hili huu ni ushindi wa Tanzania kiujumla, mashabiki pamoja na Serikali ambayo inanipa sapoti,” amesema.
SOMA NA HII  SIMBA YAZITAKA POINTI TATU ZA KMC