YANGA inayonolewa na Kocha Mkuu, Cedric Kaze baada ya kusaini dili la miaka miwili, jana Oktoba 16 mtambo wa kutengeneza mabao Kwenye kikosi hicho ni Carlos Carinhos raia wa Angola.
Kiungo huyo amehusika Kwenye mabao matatu kati ya saba ambayo yamefungwa na Yanga ndani ya Ligi Kuu Bara.
Alimpa pasi zote mbili Lamine Moro ilikuwa ni Kwenye mchezo dhidi ya Mbeya City na Mtibwa Sugar wakati Yanga ikishinda bao 1-0 Kwenye mechi zote mbili.
Bao lake la Kwanza alifunga Oktoba 3 Uwanja wa Mkapa wakati Yanga ikishinda mabao 3-0 alipewa pasi na Deus Kaseke.
Kwenye mechi hizo tano za Ligi Kuu Bara, Yanga ilikuwa inanolewa na Kocha Mkuu, Zlatko Krmpotic ambaye alifutwa kazi Oktoba 3.