Home Uncategorized PRINCE DUBE WA AZAM AINGIA ANGA ZA SIMBA NA CASABLANCA

PRINCE DUBE WA AZAM AINGIA ANGA ZA SIMBA NA CASABLANCA


IMEELEZWA kuwa nyota wa Klabu ya Azam FC, Prince Dube ameingia kwenye anga za Klabu ya Raja Casablanca ambayo inahitaji kuinasa saini yake.


Casablanca inapigana vikumbo na Klabu ya Simba ambayo nayo inatajwa kumpigia hesabu Dube.


Ofa ya Casbalanca inatajwa kuwa ni nono hivyo ikwa itawekwa mezani Simba ina kazi ya kujipanga kupindua dili hilo.

  Ofisa Habari wa Simba hivi karibuni alisema kuwa miongoni mwa nyota ambao wanaweza kupambania namba ndani ya Klabu ya Simba kutoka ni pamoja na Dube ambaye ni kinara wa utupiaji.


Ametupia mabao matano na ana pasi mbili za mabao zote alimpa mshikaji wake Obrey Chirwa.


Ofisa Habari wa Azam FC ambaye amekuwa na ushirikiano mkubwa na vyombo vya Habari, Zakaria Thabit amesema kuwa hizo ni tetesi tu.

SOMA NA HII  SIMBA WATOA NENO KUHUSU ISHU YA DAVID MOLINGA