Home Uncategorized SIMBA WATOA NENO KUHUSU ISHU YA DAVID MOLINGA

SIMBA WATOA NENO KUHUSU ISHU YA DAVID MOLINGA


KUTOKANA na mchezaji wa Yanga, David Molinga kudai kuwa ameachwa kutokana na kutowekwa kwenye orodha ya wachezaji walioelekea Shinyanga kuvaana na Mwadui FC, uongozi wa Simba umewajibu wapinzani wao Yanga kimtindo.

Haji Manara kupitia ukurasa wake ameandika namna hii:-“Molinga kawakosea nini? Why kila mara wanamuonea yeye ? 

“Unawezaje kumtendea hivyo top score wako wa ligi?Wachezaji wa bongo mnajifunza kitu. Huwa wanasajili kwa mbwembwe baadae hata safari wanawaacha.”

Molinga ametupia mabao nane kati ya 31 yaliyofungwa na Yanga kwenye ligi msimu huu. Yanga itamenyana na Mwadui FC, Juni 13 Uwanja wa Kambarange.

SOMA NA HII  VIDEO: ALICHOKISEMA ENG: HERSI BAADA YA KUTUA NA KISINDA, MUKOKO | ATAJA MAJEMBE MAPYA