Home Uncategorized RATIBA YA MECHI ZA LIGI KUU BARA LEO OKTOBA 19

RATIBA YA MECHI ZA LIGI KUU BARA LEO OKTOBA 19


LIGI Kuu Tanzania Bara inaendelea leo Oktoba 19 kwa timu nne kushuka uwanjani kusaka pointi tatu muhimu ndani ya uwanja.


Ratiba ipo namna hii:-


JKT Tanzania iliyo nafasi ya 16 na pointi nne itamenyana na Tanzania Prisons iliyo nafasi ya 12 na pointi 5, Uwanja wa Jamhuri, Dodoma saa 8:00 mchana.


Mtibwa Sugar iliyo nafasi ya 13 na pointi tano itamenyana na Namungo FC iliyo nafasi ya nane na pointi tisa, saa 10:00 jioni.


Coastal Union iliyo nafasi ya 14 na pointi tano itamenyana na Biashara United iliyo nafasi ya nne na pointi 13, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.Saa 10:00 jioni.


Polisi Tanzania iliyo nafasi ya saba na pointi 10 itamenyana na Gwambina FC iliyo nafasi ya 10 na pointi 7, saa 10:00 jioni.



SOMA NA HII  KAKOLANYA ATOA TAMKO JUU YA NAFASI YAKE SIMBA