Home Uncategorized YANGA YAIFUATA BIASHARA UNITED

YANGA YAIFUATA BIASHARA UNITED

 


KIKOSI cha Yanga leo Oktoba 30 kimeondoka Mwanza kwenda Musoma kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuchezwa kesho, Oktoba 31.


Mchezo huo utachezwa Uwanja wa Karume, Mara utakuwa ni wa nane kwa Yanga huku ukiwa ni wa tisa kwa Biashara United.


Timu zote mbili zipo ndani ya tano bora jambo linalomaanisha kwamba zote kwa msimu wa 2020/21 zipo vizuri na zitapambana kupata matokeo ndani ya uwanja.


Biashara United ambao ni wenyeji wapo nafasi ya tatu na kibindoni wamekusanya pointi 16 Yanga wapo nafasi ya pili wakiwa na pointi 19.


Kwa mujibu wa Meneja wa Yanga, Hafidh Saleh amesema kuwa wachezaji wote wapo fiti isipokuwa nyota wao Haruna Niyonzima ana sumbuliwa na malaria.


Kocha wa Biashara United, Francis Baraza amesema kuwa wapo tayari kwa ajili ya mchezo huo wa kesho.

SOMA NA HII  KUKOSA NAFASI YA KUTINGA FAINALI, KIPA MANCHESTER UNITED APEWA ZIGO LA LAWAMA