Home Uncategorized MPANGO WA SVEN NA KOSI LAKE DHIDI YA YANGA UPO HIVI

MPANGO WA SVEN NA KOSI LAKE DHIDI YA YANGA UPO HIVI


 BAADA ya kutumia dakika 180 kuokota mabao mawili kwenye nyavu zao, mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Bara, Simba leo wanakaribishwa na watani zao wa jadi, Yanga Uwanja wa Mkapa.


Kwenye mechi hizo mbili ilikuwa mbele ya Tanzania Prisons 1-0 na Ruvu Shooting 1-0 nyota wao Clatous Chama hakuwa sehemu ya kikosi ila aliporejea mchezo wake wa kwanza ilikuwa dhidi ya Mwadui FC na alianza kikosi cha kwanza Simba ilishinda mabao 5-0.


Leo kazi inatarajiwa kuanza saa 11:00 Uwanja wa Mkapa, Simba wao chini ya Kocha Mkuu, Sven Vandenbroeck wanatarajiwa kupanga kikosi chao kama ifauatavyo: Beno Kakolanya

 Shomari Kapombe

Muhammed Hussein ‘Tshabalala’

 Pascal Wawa

 Joash Onyango

 Gerrard Mkude

 Luis Miquissone

 Mzamiri Yassin

 John Bocco 

Larry Bwalya 

 Clotaus Chama


Chanzo: Championi Jumatano

SOMA NA HII  DANI ALVES ATIMKA MAZIMA PSG