Home Uncategorized CAF YAFUTA MCHEZO DHIDI YA AL RABITA V NAMUNGO FC

CAF YAFUTA MCHEZO DHIDI YA AL RABITA V NAMUNGO FC

 


MCHEZO wa Kombe la Shirikisho kati ya Sudani Kusini na Namungo FC wa marudio kwenye Kombe la Shirikisho ambao ulipaswa uchezwe leo Desemba 6 umefutwa na Caf.


Uamuzi huo umetokana na Chama cha Mpira cha Sudan Kusini (SSFA) kushindwa kukamilisha taratibu kuhusu waamuzi waliopangwa kuchezesha mechi.


Mchezo wa kwanza uliochezwa Uwanja wa Azam Complex, Namungo ilishinda mabao 3-0 ambapo mawili yalifungwa na Stephen Sey na moja na Shiza Kichuya hivyo leo ilikuwa inahitaji sare ama ishinde ili ipenye hatua ya mtoano.


Kwa kuwa mchezo umefutwa basi Namungo inapeta mpaka hatua ya mtoano Kombe la Shirikisho Afrika.


Taarifa imeeleza namna hii:-


 

SOMA NA HII  HARMONIZE AZIDI KUUMIZA VICHWA WATU, WCB WATOA TAMKO JINGINE JUU YAKE - VIDEO