MKURUGENZI Mtendaji wa Klabu ya Simba,(CEO) Barbara Gonzalez amesema kuwa suala la Shiza Kichuya limesitishwa kwa kuwa Fifa walijua kwamba wanawasiliana na mtu ambaye hayupo ndani ya Simba.
Barbara kuhusu suala hilo amesema:-“Suala la Kichuya, Fifa wanatutendea haki. Tuliwaandikia na kuwaambia hatushirikishwa lolote na kulikuwa na mtu anawasiliana na Fifa nje ya klabu.
“Sasa tunasubiri barua ya Fifa kwa maana ya mashitaka na wametuandikia barua kuwa tuendelee na shughuli zetu, Shiza ni mchezaji huru na Simba inaweza kuendelea kusajili.
“Fifa nao waligundua waliyekuwa wanawasiliana naye si mtendaji wala kiongozi wa Simba na Kichuya unaona anaendelea hadi hapo tutakapopokea barua kutokea Fifa,” .
Kwa sasa Kichuya anaendelea na maisha yake ndani ya Klabu ya Namungo FC ambayo inashiriki Kombe la Shirikisho Afrika.