Home Uncategorized SIMBA YAPIGA HODI CAF

SIMBA YAPIGA HODI CAF


 LICHA ya Simba kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Plateau United, lakini Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez, amelitaka Shirikisho la Soka Afrika (CAF) kupitia upya vigezo vilivyotumika kuruhusu mchezo wao huo kuchezwa kwenye Dimba la New Jos, Nigeria

wakati uwanja huo haujakidhi viwango vinavyohitajika.


Wikiendi iliyopita, Simba ikiwa ugenini, iliibuka na ushindi huo katika mchezo wa awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika. Timu hizo zinatarajiwa kurudiana wikiendi hii jijini Dar.


Barbara alisema kwenye kanuni na taratibu za CAF zinaelekeza aina gani ya uwanja unaotakiwa kupewa leseni ya kuchezewa michezo ya Ligi ya Mabingwa Afrika na Kombe la Shirikisho Afrika kama vile ubao wa

kieletroniki kwa ajili ya kuonyesha matokeo, dakika na vitu vingine muhimu ambavyo Uwanja wa Jos hauna.


Akiuzungumzia uwanja huo, Barbara alisema: “Kuna mapungufu mengi sana ambayo uwanja wa Jos unafanya ukose sifa ya kupewa leseni

ya kutumika katika michezo ya kimataifa. Kanuni za CAF zipo wazi, lazima uwanja uwe

na eneo bora la kuchezea, vyumba vya

kubadilishia nguo, ubao wa ‘electronic’ na vitu

vingine vingi ambavyo uwanja huu wa

umekosa.


“Sasa CAF inabidi waweke wazi na watuambie

ni vigezo gani ambavyo vilitumika hadi

kuruhusu na kutoa kibali kwa Uwanja wa Jos

kutumika kwa michezo ya kimataifa.”


KAULI YA TFF

Naye Mwenyekiti wa Mashindano wa Shirikisho

la Soka Tanzania (TFF), Ahmed Mgoi ambaye

alikuwa mkuu wa msafara wa Simba

uliokwenda nchini Nigeria, alisema: “Mapungufu

yaliyojitokeza kwenye mchezo huo hayana

nafasi tena, kwa sababu mechi ya kwanza

imekwisha na wameshinda, kikubwa Simba

wajipange kwa ajili ya mchezo ujao ili wafanye

vizuri na kusonga mbele.”


KUREJEA LEO

Meneja wa Simba, Abbas Ally, alisema kikosi

kilianza safari jana Alfajiri kutoka Jos, Nigeria

kupitia Ethiopia na kinatarajia kutua kwenye

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro

majira ya saa 10:00 jioni.

“Tunashukuru kwa kuanza vizuri michuano hii

mikubwa kwa ngazi ya klabu barani Afrika, licha

SOMA NA HII  YANGA V COASTAL UNION LEO NI MOTO KWA MKAPA

ya matokeo ya ushindi tuliyoyapata nikiri kuwa

haukuwa mchezo rahisi kutokana na ubora wa

wapinzani wetu na hata mazingira ya mchezo,

lakini wachezaji wetu walipambana.