Home Uncategorized TANO BORA YA WAFUNGAJI BONGO

TANO BORA YA WAFUNGAJI BONGO


LIGI Kuu Bara msimu wa 2020/21 imezidi kuchanja mbunga huku vita kila seheu ikiwa ni ya moto kwa timu na mchezaji mmoja ndani ya timu.


Vita ya ufungaji nayo pia inazidi kupamba moto ambapo kwa msimu uliopita kiatu kilisepa na kuibukia Simba kwa mshambuliaji, Meddie Kagere ambaye alifunga jumla ya mabao 22.

Kwa msimu huu tayari Kagere ametupia mabao manne ndani ya Simba huku akizidi kupewa nafasi ya kufanya vizuri licha ya kukwama kuona nyavu kwenye mechi mbili za hivi karibuni.

Kwa sasa kinara wa utupiaji ni John Bocco ambaye amefunga jumla ya mabao 8, huyu pia ni nahodha wa Simba.

Adam Adam ni nyota anayekipiga ndani ya JKT Tanzania ametupia jumla ya mabao 7.

Prince Dube,staa wa Azam FC alianza kwa kasi kabla ya kupata majeraha ambayo yamemuweka nje ya uwanja ametupia jumla ya mabao 6. 

Meshack Abraham ni mali ya Gwambina FC kibindoni ametupia jumla ya mabao 6. 

Clatous Chama kiungo nyota wa Simba yeye ametupia jumla mabao 6.

SOMA NA HII  YANGA NI BALAA, YAIKIMBIZA SIMBA NA AZAM KINOMA