Home Uncategorized MUANGOLA WA YANGA MAJANGA MATUPU

MUANGOLA WA YANGA MAJANGA MATUPU


 KIUNGO wa Yanga, Carlos Fernandes ‘Carlinhos’ amepata majanga akiwa na kikosi cha timu hiyo visiwani Zanzibar ambapo amerudishwa jijini Dar na kuikosa michuano ya Kombe la Mapinduzi inayoendelea visiwani humo.

Akizungumza na Spoti Xtra, Ofisa Habari wa Yanga, Hassan Bumbuli, alisema: “Kikosi kipo vizuri, wachezaji wote wapo fiti isipokuwa Carlinhos ambaye amerejeshwa Dar.“

 

Anatakiwa kuendelea na matibabu pamoja na program alizokuwa amepangiwa kutokana na kutokuwa fiti.”


Kikosi cha Yanga jana kilifanya mazoezi ya mwisho kwa ajili ya kujiaandaa na mchezo wa leo dhidi ya Namungo FC.


Mchezo wa kwanza Yanga ililazimisha sare ya bila kfungana na Klabu ya Jamhuri ambapo nyota huyoo raia wa Angola hakuwepo benchi. 

SOMA NA HII  TRENT ALEXNDER WA LIVERPOOL NJE KIKOSI CHA TIMU YA TAIFA YA ENGLAND