Home Uncategorized YANGA NA SIMBA ZAPIGANA VIKUMBO KUPATA SAINI YA BEKI HUYU WA KUSHOTO

YANGA NA SIMBA ZAPIGANA VIKUMBO KUPATA SAINI YA BEKI HUYU WA KUSHOTO


 IMEELEZWA kuwa mabosi wa mitaa ya Kariakoo, Simba na Yanga wanapiga hesabu ya kuipata saini ya nyota wa Klabu ya Namungo, Edward Charles Manyama ili kuinasa saini yake.

Yanga walifungua njia ya kuwasiliana na beki huyo ambaye amecheza ndani ya timu hiyo ghafla Simba nao wanatajwa kuanza mazungumzo.


Simba wanahitaji beki wa kushoto ambaye atakwenda kumpa changamoto Mohamed Hussein baada ya Gadiel Michael mambo kwake kuwa magumu.

Yanga inahitaji kuweka ukuta chuma kwa kila atakayekuwa nje na atakayekuwa ndani kwa msimu wa 2020/21.
Beki huyo mzawa amesema kuwa ikiwa kuna timu zitahitaji saini yake yeye ataangalia maslahi pamoja na nafasi yake ya kucheza.
SOMA NA HII  TSHISHMIBI NA FEI TOTO WAMVUTA NDANI YA YANGA KIUNGO MKALI WA KENYA