KIUNGO mshambuliaji wa Simba, Larry Bwalya amesema kuwa timu hiyo ina nafasi kubwa ya kufanya maajabu katika Hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambayo inatarajiwa kupangwa leo Ijumaa.
Bwalya alijiunga na Simba mwanzoni mwa msimu huu amekuwa ni chaguo la kwanza la Kocha Mkuu, Didier Gomes, raia wa Ufaransa.
Akizungumza kuelekea kwa droo hiyo ambapo Simba ndiyo itajua mpinzani wake, Bwalya alisema: βImekuwa heshima kwangu na timu pia kuona tunafanikiwa kutinga hatua ya robo fainali katika michuano ya kimataifa.
βKwa sasa tunasubiri ratiba na timu ambayo tutacheza nayo katika hatua ya robo fainali ya michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
βBado tunayo nafasi ya kutwaa ubingwa wa michuano hiyo kutokana na maandalizi mbalimbali ambayo tunaendelea kufanya, β alisema Bwalya.
Katika droo ya leo Simba inatarajiwa kupangwa na wapinzani kati ya hawa, CR Belouizdad au MC Alger zote za Algeria au Kaizer Chiefs ya Afrika ya Afrika Kusini inatarajiwa kupangwa saa 9:00 alasiri.