Home kimataifa MBAPPE: KUHUSU MKATABA WANGU, SUBIRINI KWANZA

MBAPPE: KUHUSU MKATABA WANGU, SUBIRINI KWANZA


 KYLIAN Mbappe nyota wa kikosi cha PSG imeelezwa kuwa atatoa hatma yake ndani ya kikosi hicho baada ya kumalizika michuano ya Euro 2020.

Licha ya kutajwa kuwaniwa na timu mbalimbali, nyota huyo bado hajasaini mkataba mpya ndani ya kikosi hicho.

Miongoni mwa timu ambazo zinatajwa kuwania saini yake ni pamoja na Liverpool, Manchester City na Manchester United.

Mkataba wake unatarajiwa kumeguka Juni 2022 na klabu kwa sasa lengo lake ni kumpa mkataba mrefu na kwa wakati huu wapo kwenye mazungumzo.

Mbappe amesema:”Kwa sasa ninafurahi taji langu ndiyo jambo muhimu sababu tumeweka juhudi kufanikiwa, kuhusu kusubiri mkataba tusubiri,”.

SOMA NA HII  ROMELU LUKAKU ANA TUZO MBILI ZA UFUNGAJI BORA