PRINCE Dube leo Juni 26 alikuwa Uwanja wa Majimaji, Songea akishuhudia mchezo wa nusu fainali uliowakutanisha Azam FC dhidi ya Simba na kushuhudia timu yake ikipoteza kwa kufungwa bao 1-0. Akiwa jukwaani mashabiki walimfuata na kuanza kupiga naye picha za ukumbusho kinara huyo wa mabao ndani ya ligi kwa Azam FC akiwa na mabao 14.