BREAKING: UONGOZI wa Azam FC leo Julai 31 imemtangaza nyota mpya Idrisa Sembombo raia wa Congo ambaye ni mshambuliaji.
Nyota huyo amesaini dili la miaka miwili kwa ajili ya kuitumikia timu hiyo inayotumia Uwanja wa Azam Complex.
Ameibuka ndani ya Azam FC akitokea Klabu ya El Gouna ya Misri hivyo atakuwepo mpaka 2023.
Pia aliwahi kucheza ndani ya Klabu ya Nkana FC ambayo Mtanzania Hassan Kessy ambaye kwa sasa yupo Mtibwa Sugar aliwahi kuitumikia.