Home Habari za michezo KUHUSU MSEMAJI MPYA YANGA….BABA LEVO NAYE AJITOSA KUOMBA NAFASI…AHAIDI KUWAKERA MSIMBAZI…

KUHUSU MSEMAJI MPYA YANGA….BABA LEVO NAYE AJITOSA KUOMBA NAFASI…AHAIDI KUWAKERA MSIMBAZI…

Kutoka kwa chawa wa kimataifa Babalevo jana amethibitisha kuwa ametuma maombi ya Usemaji kwenye Klabu ya Yanga.

Ikumbukwe Siku chache zilizopita Klabu hiyo iliachana na Msemaji wao, Hassan Bumbuli baada ya kumaliza mkataba wake, hivyo nafasi hiyo ipo wazi kwa sasa.

Kupitia Ukurasa wa Instagram Baba levo ameshare picha yenye ujumbe uliothibitisha kuwa Barua yake ya Maombi tayari imeshafika katika Ofisi za Klabu hiyo;

“Lengo ni kuhakikisha timu ya wananchi Yanga hatupoi. Ni wahahakishie tuu hakuna walichokiepuka kero itakuwa vilevile 100%,” ameandika Baba Levo

SOMA NA HII  NJIA YA YANGA KUTOBOA MAKUNDI CAF HII HAPA....WAKISHINDWA NA HII NDIO BASI TENA...