Home Habari za michezo #SIKUYAWANANCHI:…YANGA WADHIHIRISHA UKUBWA WAO…..MASHABIKI WAFURIKA ‘POMONI’ KWA MKAPA…TAMBO ZATAWALA…

#SIKUYAWANANCHI:…YANGA WADHIHIRISHA UKUBWA WAO…..MASHABIKI WAFURIKA ‘POMONI’ KWA MKAPA…TAMBO ZATAWALA…


Kadiri muda unavyozidi kusogea ndivyo ambavyo Mashabiki wa Dar Young Africans wanavyozidi kumiminika katika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam katika kuadhimisha siku ya Mwananchi.

Japokuwa hapo awali mwamko wa mashabiki ulionekana ni mdogo lakini hali ilivyo mpaka kufikia mida ya saa nane mchana tayari Uwanja umetapika.

Kwa sasa inafuata mechi ya Kirafiki kati ya Yanga Princess dhidi ya Ilala Queens, na majira ya saa moja usiku ni Yanga dhidi ya Vipers SC.

SOMA NA HII  MBALI NA KUPATA TIMU UARABUNI HUKO...MSUVA ANENDELEA KUIOTA YANGA...AWATUMIA UJUMBE HUU WA MATUMAINI...