Home Habari za michezo WAKATI YANGA SC WAKIENDELEA KUKAZA…FEI TOTO ATUA KWA ‘WAARABU’ KULA MAISHA…

WAKATI YANGA SC WAKIENDELEA KUKAZA…FEI TOTO ATUA KWA ‘WAARABU’ KULA MAISHA…

Tetesi za Usajili Yanga

Kiungo mahiri wa Tanzania aliyetangaza kununua mkataba wake na Yanga SC ya Dar es Salaam, Feisal Salum Abdallah ‘Fei Toto’ yupo Dubai, Falme za Kiarabu akiwa katika mapumziko na katika sherehe za kuukaribisha Mwaka mpya.

Mwanandinga huyo ametua Dubai jana asubuhi akitokea Visiwani Zanzibar na kupokelewa na wenyeji wake.

”Tumempokea Fei Toto, tutakuwa naye hapa Dubai amekuja kupumzika,” amesema mmoj kati ya wadau wakubwa waliofika kumpokea, ambaye hakupenda jina lake litajwe.

”Sina nilichosahau, kwa sasa nipo hapa Dubai kupumzika baada ya hapo nitaamua timu gani niende kucheza mpira,” alisema kiungo huyo.

Feisal ambaye pia ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ alitangaza kununua mkataba wake na Yanga, lakini uongozi wa Yanga umekataa suala hilo na kusisitiza kuwa kiungo huyo bado mchezaji halali wa Yanga SC na mkataba wake utamalizika Mei mwaka 2024.

SOMA NA HII  PAMOJA NA KUFUNGIWA VIOO MSIMBAZI...MORRISON AIBUKA NA MPANGO WA KUIPELEKA SIMBA GHANA...AOMBA MSAADA..