Habari za Yanga SC
Habari za michezo

WAKILI SAIMON:- WAMEFANIKIWA KUMUHARIBIA FEI TOTO MAISHA YAKE…YANGA IMEPOTEZA MCHEZAJI…

admin March 11, 2023 2:49 pm

Mwanasheria wa Klabu ya Yanga, Wakili Patrick Simon amesema kuwa waliomrubuni mchezaji wao Feisal Salum ‘Fei Toto’ kutaka kuvunja mkataba wamefanikiwa kumharibia taaluma yake na maisha yake ya mbeleni.

Kauli hiyo ya Patrick inakuja ikiwa ni baada ya kiungo huyo kutoka Zanzibar amegonga mwamba kwa mara ya pili, mbele ya Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Soka nchini Tanzania ‘TFF’.

Kutoka kwenye ukurasa wa Twitter ya wakili Simon, ameandika;

“Mtazamo Wangu:

– Yanga imepoteza mchezaji wake. – Kijana kapoteza nafasi ya kucheza mpira. – Aliyenyuma ya kijana kafanikiwa kumuharibia maisha. – Familia ya Kijana imenufaika kimaisha. – Wanasheria wa Kijana wamejitengenezea pesa. – Waandishi wamefanikiwa kutengeneza Content.”

Feisal aliomba kurejewa kwa maamuzi ya shauri lake dhidi ya Yanga, lakini bado Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ikaendelea kusimamia msimamo wake wa kumtambua kama Mchezaji halali wa Klabu hiyo ya Jangwani.

Feisal alitangaza hadharani kuvunja mkataba na Young Africans mwishoni mwa mwaka 2022, lakini baadae Uongozi wa Klabu hiyo ulimshtaki TFF kwa kushinikiza arejee kambini kujiunga na wenzake lakini haikuwa hivyo.

Je, una maoni gani kuhusu sakata la fei Toto na Yanga.

KISA KUWA NA TABIA ZA UBINAFSI…NABI AMPA MAKAVU LIVE MAYELE…ISHU IKO HIVI… MANARA ASHTUKIA JAMBO YANGA…AMNYOOSHEA KIDOLE MAYELE…AONYA YA FEI TOTO…

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6131

Leave a Reply