Machi 13 Kikosi cha Wachezaji 31 cha Timu ya Taifa kilitangazwa kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kufuzu AFCON dhidi ya Timu ya Taifa ya Uganda.
Mbali na kuitwa kikosi hicho kuna wachezaji wamekosekana akiwemo mlinzi wa kushoto wa Simba SCMohammed Hussein “Tshabalala”
Wengi wamehoji kukosekana kwa beki huyo ambae yupo kwenye ubora wa juu kwa sasa, lakini Mchambuzi wa Soka Geoff Lea amesema kwake yeye sio jambo la ajabu kutoitwa kwa mchezaji huyo.