KOCHA Mkuu wa Azam FC, Kally Ongala ameichifua kuwa, kwenye timu hiyo hakuna supastaa na mchezaji yeyeote anaweza kuanzia benchi na bado timu ikapata ushindi kama kawaida.
Kauli ya Ongala imejiri baada ya kuwaweka baadhi ya wachezaji wa timu hiyo benchi juzi usiku wakati Azam ikiizamisha tena Mtibwa Sugar kwenye mechi ya Ligi Kuu Bara iliyopigwa Azam Complex, akiwemo Prince Dube na Kipre Junior ambao ni tegemeo wa kikiosi hicho.
“Unapokuwa na wimbi la wachezaji wengi bora unaamua leo aanze huyu na kesho yule kwa sababu hawatofautiani sana na hilo ndilo ambalo sisi kama benchi la ufundi tulikuwa tunalihitaji kutokana na kushiriki mashindano mengi.”