Home Habari za michezo WAKATI SIMBA WAKITAMBA NA BEKI WAO MCAMEROON…YANGA WAMESHUSHA CHUMA HIKI CHA KAZI…

WAKATI SIMBA WAKITAMBA NA BEKI WAO MCAMEROON…YANGA WAMESHUSHA CHUMA HIKI CHA KAZI…

Gift Fred atambulishwa Yanga

Beki wa timu ya taifa ya Uganda (Uganda Cranes) Gift Fred amejiunga na Mabingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara Yanga SC.

Beki huyo mahiri amesaini mkataba wa miaka mitatu Ijumaa kutokana na Prosper Agency ambaye alisimamia mchakato wa uhamisho (usajili).

Gift ambaye amekuwa nahodha katika klabu ya SC Villa alionyesha kiwango kizuri msimu uliopita Jogoos walipojaribu kushinda taji la ligi na kupoteza siku ya mwisho kwa Vipers SC.

Gift alisaini na kikosi cha Tanzania kama mchezaji huru baada ya kumalizika kwa mkataba wake na SC Villa mwezi uliopita.

Pia amekuwa kwenye rada za vilabu kadhaa hasa vya Uganda (Vipers SC na Kitara FC) na Afrika Kusini.

Hivi sasa Yanga wanajiimarisha kwa kufanya usajili wa kimya kimya huku hofu ikitanda kwa mashabiki wao kuhusu sakata ;a kufungiwa kusajili na FIFA.

Itakumbukwa kuwa mapema mwishoni mwa mwezi uliopita FIFA walituma barua kwa Yanga wakiweka shinikizo la klabu hiyo kumlipa aliyekuwa kocha wao Lucy Emely ambaye alifungua shauri kwenye shirikisho hilo akitaka Yanga wamlipe pesa zake.

Hata hivyo Yanga kupitia kwa Afisa habari wake wamedai kuwa tayari wameshamlipa kocha huyo hivyo wameepukana na zuio la kusajili ambalo wangekutana nalo.

Hata hivyo, si TFF wala Yanga wenyewe waliotoka tena hadharani kuelezea sakata hilo, zaidi ya kuwepo kwa tetesi za kwenye mitandao ya kijamii.

Yanga ndio mabingwa watetezi wa Ligi kuu Tanzania, pamoja na kombe la shirikisho la TFF huku pia wakiumaliza msimu uliopita kwa kufika Fainal ya kombe la Shirkisho Afrika.

SOMA NA HII  NABI BAADA YA KUSKIA SIMBA WAKO BENIN...KACHEEKAA KISHA AKASEMA HAYA...AOMBA DK 180 TU...