Home Habari za michezo YANGA YAMFUKUZISHA KAZI KOCHA MAZEMBE…INASIKITISHA SANA KWA UNYAMA HUU

YANGA YAMFUKUZISHA KAZI KOCHA MAZEMBE…INASIKITISHA SANA KWA UNYAMA HUU

YANGA YAMFUKUZISHA KAZI KOCHA MAZEMBE...INASIKITISHA SANA KWA UNYAMA HUU

Klabu ya TP Mazembe imemteua aliyekuwa kocha wa Timu ya Taifa Senegal, Lamine Ndiaye kuwa kocha mkuu klabuni hapo kuchukua nafasi ya mzawa Mihayo Kazembe aliyeshindwa kuiongoza klabu hiyo kufuzu kwenda robo fainali ya kombe la Shirikisho Afrika.

N’Diaye (66) raia wa Senegal ambaye aliiongoza Mazembe kutwaa Ligi ya Mabingwa Afrika mnamo 2010, amewahi kuvinoa vya Mulhouse (1998), Coton Sport (2003-2006), Maghreb Fez (2008- 2009), TP Mazembe (2010-2013), Al-Hilal (2018-2019) na Horoya AC (2019-2022)

Mwishoni mwa mwaka 2022, Kocha huyo alihusishwa kujiunga na Simba SC, siku chache baada ya kuondoka Horoya AC ya Guinea, lakini baadae Wekundu hao wa Msimbazi walimtangaza Kocha Robertinho.

SOMA NA HII  SABABU YA DITRAM NCHIMBI KUTOFUNGA HII HAPA